• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Baraza maalumu la kujadili hoja za CAG

Posted on: July 2nd, 2024

HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI YAPATA HATI SAFI .

Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara imepata hati safi kwa miaka mitano (5) mfululizo huku Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akiipongeza Halmashauri hiyo na kusema kuwa imetimiza  kwa vitendo agizo la Serikali Kwa asilimia 100%.

Hati hiyo safi ni muendelezo wa upatikanaji wa Miaka mitano mfululizo kuanzia mwaka 2018/2019.

Hayo yameelezwa Leo julai 02/2024 Katika kikao maalumu Cha Baraza la Madiwani Cha kujadili na kupitia hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2022/2023 kilichofanyika Katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo  Mbuyuni Masasi.

Akizungumza katika baraza hilo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenani Sawala, Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe.Lauteri John Kanoni amesema "Mkuu wa Mkoa wa Mtwara anawapongeza sana Kwa kupata hati safi kwa muda wa miaka mitano mfululizo, pili anampongeza mwenyekiti na  Kamati yake, Pamoja na Watendaji kwa kujibu hoja nyingi ambazo zimetoka  kwenye hoja 18 na kubakiwa na hoja 4 ni umahiri mkubwa hivyo anaamini kwa mwaka ujao hoja zote zitamalizika, hongereni sana".

"Pia nawapongeza  waheshimiwa Madiwani kwasababu nyie ndio mnaotoa maamuzi ya kuhakikisha mnatekeleza kwa vitendo yale maelekezo ya Serikali yakupeleka fedha kutokana na mapato ya ndani ili  ziende kwenye Shughuli za maendeleo kwaiyo mmewatendea  vyema wapiga kura wenu.

Aidha mhe.kanoni Katika kuhitimisha taarifa yake ametumia nafasi hiyo Kutoa maelekezo kwa Halmashauri kuwa, "katika mwaka huu mpya wa fedha ulioanza,  Mkuu wa Mkoa hapendi kuona katika mkoa wa Mtwara  mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan analeta fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo na hatmaye kushindwa kutumia fedha hizo kwa wakati alafu zinarudi tena Serikalini  lazima tutambue kuwa hatuwatendei haki Wananchi,  hivyo kuanzia mwaka huu wa fedha ulioanza mjipange fedha zote mnazozipata zitumike ipasavyo na kuhakikisha zinamalizika.

Beatrice Mwinuka ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, awali akiwasilisha taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2022/2023 amesema Katika kutekeleza jukumu lake la kisheria chini ya ibara 143 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kifungu cha 10, kifungu kidogo cha kwanza, na Sheria ya ukaguzi wa umma kifungu namba 148, Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za Serikali Kwa mwaka wa fedha ulioishia june 30, alikagua Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Kutoa maoni yake huru.

Amesema katika utoaji wa maoni ya Mdhibiti na Mkaguzi kwa mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30/06/2023 alikagua mahesabu ya Halmashauri na kupitia majibu ya hoja kutoka timu ya Menejimenti na hatmaye Kutoa hati safi.

Mwinuka ameongeza kuwa, utekelezaji wa hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali Kwa mwaka 2022/2023 kwa Mwaka huo Ofisi ya CAG ilitoa mapendekezo 18, ambapo hoja 14 zimefanyiwa kazi na kufungwa na hoja 4 zipo kwenye utekelezaji, na pia kulikuwa na maagizo nane (8) kutoka Kamati ya bunge, 6 yamejibiwa na mawili yapo kwenye utekelezaji.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Ndg.Ibrahimu Chiputula amesema Halmashauri hiyo imeendelea kufanya vizuri na kupata hati safi kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo ni kutokana na kazi kubwa ambayo wanaifanya wao na Watendaji kwa Umoja (team) hivyo anawashukuru na kuwapongeza sana, 

"pongezi hizi ambazo zitatolewa kwa kupata hati safi ni kazi kubwa tunayoifanya sisi na Watendaji wetu, hivyo niendelee kuwaomba Wataalamu tunapoletewa fedha za miradi tuhakikishe hazirudi hazina bali zinatumike zote kwani katika Maeneo yetu bado Kuna miradi mingi ambayo inahitaji kutekelezwa.

Imeandaliwa na: 

Winifrida Ndunguru -Afisa Habari Masasi DC

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa