• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

AFISA AFYA MAZINGIRA: HAKIKISHENI MNAJENGA NA KUTUMIA VYOO BORA ILI KUEPUKA KUPATA MAAMBUKIZI YA MAGONJWA.

Posted on: September 28th, 2025


Na:Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini (H/W) Masasi.


Nyumba ni Choo! Huu ni usemi ambao hutumika mara nyingi ukiangazia umuhimu wa choo bora na huduma za kujiweka safi nyumbani.


Choo kinaweza kuwa sehemu ya kawaida mathalani shimo refu katika ardhi, lakini kutokana na mahitaji ya faragha ni muhimu choo kuwa na kijumba na mlango.Banda au kijumba kinaweza kutengenezwa kutokana na vifaa vya kawaida, au kutokana na mchanga au saruji.


Usafi katika jamii ni muhimu sana kama ulivyo

kwa mtu binafsi na familia, usafi wa Mazingira humainisha usafi wa jamii kutumia vyoo safi na salama, kulinda usafi salama wa vyanzo vya maji na utupaji salama wa taka, huku suala la uchafuzi wa Mazingira inaelezwa husababisha magonjwa na vifo vingi ambavyo vingeweza kuepukika.


Juhudi yeyote ile ya jamii kwa ajili ya kuboresha usafi wa Mazingira lazima iwasidie watu kuondokana na changamoto zinazowakabili katika maisha yao ya kawaida.


Na ndio maana kwa kulitambua hilo, timu ya Wataalamu kutoka Idara ya Afya kwa kushirikiana na Kitengo cha Udhibiti wa taka na usafi wa Mazingira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mapema tarehe 26 Septemba 2025 ikiwa ni siku ya Afya Mazingira duniani, ilifanya  mkutano na wananchi wa Kijiji cha Mbuyuni huku lengo kubwa likiwa ni kuwapa elimu juu ya masuala mbalimbali yanayoendana na uchafuzi pamoja na usafi wa Mazingira.


Bw.Said Ame ni Afisa Afya Mazingira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Masasi akizungumza katika mkutano huo amesema jamii inatakiwa ihakikishe inajenga na kutumia vyoo bora ili kuepuka kupata maambukizi ya magonjwa ya mlipuko na kujenga tabia ya kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na kuendelea kuimarisha usafi wa Mazingira kwa kila kaya.

Amesema takwimu zinaonyesha kuwa katika kijiji cha Mbuyuni kilichopo katika Kata hiyo ya Mbuyuni

kaya nyingi hazina vyoo hivyo kupelekea choo kimoja kinachangiwa na kaya zaidi ya mbili hadi tatu.


"Kila ifikapo tarehe 26 Septemba kila mwaka huwa tunafanya maadhimisho ya siku ya Afya Mazingira duniani, hiki tunachokifanya hapa kwenu na hata maeneo mengine tunafanya, lakini kwa kata yote ya Mbuyuni na hasa kijiji hiki cha mbuyuni  takwimu zake za usafi sio nzuri sana hivyo  bado mnakazi ya kufanya ili kuendelea kutunza afya zetu'."

"Lazima tufahamu Mazingira yana uhusiano moja kwa moja na afya ya binadamu, Mazingira yasipokuwa safi basi afya ya binadamu itatetereka

kwaiyo haya tunayoyasisitiza wala hayana gharama" alisisitiza


Aidha, ameendelea kuwakumbusha Wananchi kuachana na ujenzi wa vyoo vya nyasi ambavyo si bora na salama ambavyo kupelekea mvua zinaponyesha vyoo hivyo kuanguka na kubaki wazi sehemu ya juu na hivyo kupoteza ubora wa vyoo hivyo.

Hata hivyo pamoja na kuwataka  wajenge  vyoo kwa  kutumia vifaa vya Kudumu  Bw. Ame alihitimisha kwa kuwaelezea sifa za choo bora zikiwemo shimo refu, kiwe na mlango, kiwe na sakafu ili kiwe rahisi kusafishwa pamoja kuezekwa ili kipindi cha mvua choo kiweze kutumika.


28/09/2025

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • TUNAWAHIMIZA TUMIENI SMART TOILET KWA ULINZI WA AFYA YA MAZINGIRA: AFISA AFYA MAZINGIRA

    September 28, 2025
  • AFISA AFYA MAZINGIRA: HAKIKISHENI MNAJENGA NA KUTUMIA VYOO BORA ILI KUEPUKA KUPATA MAAMBUKIZI YA MAGONJWA.

    September 28, 2025
  • Dkt.Samia Suluhu Hassan azuru kaburi la Rais wa awamu ya tatu Hayati Benjamin William Mkapa :Lupaso

    September 24, 2025
  • SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA NA KUIMARISHA HUDUMA ZA KIJAMII: DKT.SAMIA SULUHU HASSAN

    September 24, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa